VHM

Pages

Saturday, April 12, 2014

MADHARA YA WAZAZI NA NDUGU KUMCHAGULIA MTU MUME AU MKE WA KUOLEWA NAYE


 Na Mchungaji Peter Mitimingi


1. Kuchaguliwa mwenza na wazazi. Familia nyingi za Kiafrika huwa zinavunjika kwa sababu hii.

2. Imekuwa ni kawaida hasa kwetu Waafrika kwa sababu ya urafiki wa kifamilia wazazi wa familia hizi mbili wanaweza kuamua na kuchagua wenza wa watoto wao kwa lengo la kuendeleza na kudumisha mahusiano yao kwa kupitia ndoa ya watoto wao.

3. Kuoa au Kuolewa kwa Kuwafurahisha Wanandugu. Kuoa au kuolewa kwa nia ya kutimiza matakwa ya ndugu na wanafamilia wako vilevile ni moja ya sababu zisizo sahihi za mtu kuoa au kuolewa. Ndoa sio ya ukoo ndoa ni ya watu wawili nan i lazima wakubaliane wao wenyewe bila ushawishi wa mtu wa tatu.

4. Kama ilivyo kuoa au kuolewa kunako waumiza wazazi wako, haipaswi mzazi kwa akili zake timamu amlazimishe kwa manufaa yao wenyewe binafsi, kwani itakuwa ni kumuumiza mtoto wake.

5. Hakuna mtoto ambaye kwa kufikiri kwake sawa sawa atafunga ndoa kwa minajili ya kuwaumiza wazazi wake au kuwakera. Ndoa kwa hali hiyo itakuja na changamoto zake na mambo yake, mambo mengine yanaweza kuwa ni magumu sana kuyakabili katika ndoa.

5. Kila mmoja kwa sehemu yake yaani wanaotarajia kuoana au kwa upande wa wazazi, nimuhimu kufuata taratibu zinazohusika ambazo hazitaweza kuumiza upande wowote. Let it be win-win situation. Wazazi washinde na watoto washinde pia.

0 comments:

Post a Comment